Job 9:1-6
Hakuna Mpatanishi
1Kisha Ayubu akajibu:2 a“Naam, najua hili ni kweli.
Lakini mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
3 bIngawa mtu angetaka kushindana naye,
asingaliweza kumjibu Mungu hata mara moja miongoni mwa elfu moja.
4 cHekima yake ni kubwa sana na ana uwezo mwingi mno.
Ni nani aliyempinga naye akawa salama?
5 dAiondoa milima bila yenyewe kujua
na kuipindua kwa hasira yake.
6 eAitikisa dunia kutoka mahali pake
na kuzifanya nguzo zake zitetemeke.
Copyright information for
SwhKC